Wq/sw/Nelson Mandela

From Wikimedia Incubator
< Wq‎ | sw
Wq > sw > Nelson Mandela

Nelson Rolihlahla Mandela (18 Julai 1918 - 5 Desemba 2013) alikuwa mwanasiasa nchini Afrika Kusini, kiongozi wa mapambano dhidi ya siasa ya ubaguzi wa rangi (Apartheid), mfungwa jela kwa miaka 27 halafu rais wa kwanza aliyechaguliwa kidemokrasia katika nchi yake.

Alikuwa mwanasheria na mwanachama, baadaye kiongozi wa chama cha ANC kilichopigania haki za binadamu wote nchini Afrika Kusini.

Nukuu[edit | edit source]

  • Elimu ni silaha yenye nguvu zaidi unayoweza kuitumia kubadilisha ulimwengu.
  • Iko mikononi mwako, kuufanya ulimwengu kuwa bora kwa wote wanaoishi ndani yake.
  • Mshindi ni mtu anayeota ndoto na haikatii tamaa.
  • Kushinda umaskini sio kazi ya hisani, ni tendo la haki.
  • Jambo la maana maishani si kwamba tumeishi. Bali ni tofauti gani tumeleta katika maisha ya wengine.