Wq/sw/Gertrude Mongella

From Wikimedia Incubator
< Wq‎ | sw
Wq > sw > Gertrude Mongella
Gertrude Mongella

Gertrude Mongella alikuwa Rais wa kwanza wa Bunge la Umoja wa Afrika[1]. Pia alikuwa mbunge wa jimbo la Ukerewe[2] katika bunge la taifa nchini Tanzania.

Gertrude alizaliwa mwaka 1945 katika kisiwa cha Ukerewe katika Mkoa wa Mwanza (Tanzania). Baba yake, Patrice Magologozi alikuwa fundi seremala na mwashi na mama yake, Bibi Nambona, alikuwa mkulima.

Gertrude Mongella ameshika nyadhifa mbalimbali za kitaifa na kimataifa. Miaka 1993-1995 alikuwa Katibu Mkuu wa Mkutano wa Umoja wa Mataifa wa Masuala ya Wanawake na kuhudhuria mkutano wake wa nne uliofanyika Beijing, China mwaka 1995. Amewahi kuwa balozi nchini India (1991-1993), Waziri Asiye na Wizara Maalum, Waziri wa Ardhi, Maliasili na Utalii, mshauri maalum wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni[3]

Nukuu[edit | edit source]

  • Mapinduzi ya usawa kati ya wanaume na wanawake yameanza, hakuna kurudi nyuma
    • Gertrude Mongella [1]

viungo vya njee[edit | edit source]

  1. https://sw.wikipedia.org/wiki/Bunge_la_Umoja_wa_Afrika
  2. https://sw.wikipedia.org/wiki/Ukerewe
  3. https://sw.wikipedia.org/wiki/Shirika_la_Umoja_wa_Mataifa_la_Elimu,_Sayansi,_na_Utamaduni